Posts

Showing posts from September, 2025

TANESCO YAKUTANA NA WADAU MOROGORO KUJADILI MIKAKATI YA KUTUNZA VYANZO VYA MAJI BWAWA LA JNHPP.

Image
  📌 Ni kufuatia utafiti uliofanywa na TANESCO kutambua vihatarishi na hatua za kuchukua kunusuru vyanzo  Vya mito. 📌RC Malima aongoza kikao hicho na kukubaliana hatua za kudhibiti mapema Morogoro Septemba 26,2025. Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limekutana na wadau mbalimbali kutoka taasisi za serikali, Uongozi wa Mkoa wa Morogoro, pamoja na wataalamu wa mazingira, maji na nishati, katika kikao kilichofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, kwa lengo la kujadili vihatarishi na mikakati ya kulinda vyanzo vya maji vinavyopeleka maji katika mabwawa ya kuzalisha umeme, hususani Bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere. Kikao hicho kimeongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Malima, na kuhudhuriwa na wakuu wa wilaya za Morogoro, Ulanga, Malinyi na Ifakara, pamoja na viongozi waandamizi wa TANESCO wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji, Bwana Lazaro Twange. Katika kikao hicho, wadau wamejadili kwa kina vihatarishi vinavyojitokeza sasa na ambavyo visipodhibitiwa mape...

TARURA KUJA NA TEKNOLOJIA MBADALA YA UJENZI WA BARABARA NA MADARAJA.

Image
  Na.Sophia Kingimali Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) umebuni mbinu za kutumia teknolojia mbadala katika ujenzi wa barabara na madaraja, hatua iliyosaidia kuokoa mabilioni ya shilingi za serikali na kuharakisha utekelezaji wa miradi mbalimbali nchini. Pia,TARURA inatarajia kujenga daraja kubwa kuliko yote jijini Dar es salaam ambalo litatumia zaidi ya bilioni 1.6 Akizungumza leo Septemba 26,2025 jijini Dar es salaam Mratibu wa Ujenzi kwa Teknolojia Mbadala wa TARURA, Phares Ngeleja, amesema serikali imeikabidhi TARURA jukumu la kusimamia, kujenga na kukarabati mtandao wa barabara wenye urefu wa takribani kilomita 144,429.77 kote nchini.  “Ujenzi na ukarabati wa barabara unahitaji fedha nyingi sana. Ndiyo maana TARURA tumeamua kutafuta njia nafuu zaidi ambazo zitawasaidia wananchi kupata barabara na madaraja kwa gharama ndogo lakini zenye ubora unaokubalika,” amesema Ngeleja. Ngeleja amesema madaraja ni kiungo muhimu katika barabara yoyote, hivyo TARURA imewek...

WAZAZI ZANZIBAR WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA YA ELIMU BURE.

Image
  WAKAZI wa Zanzibar wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuchangamkia fursa iliyotolewa na chuo cha VETA FURAHIKA kwa wazazi kuwapeleke watoto wao chuoni hapo ili wapate elimu bure itakayowafaa katika maisha yao na kuwaondoa katika hatari ya kujiunga katika makundo ovu ya uasherati. Dkt. David Msuya ambaye ni Mkuu wa Chuo Cha Ufundi Furahika jijini Dar es Salaam ametoa wito huo leo, Septemba 26, 2025 wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake na kubainisha kwamba masomo katika chuo hicho ambacho kipo Kituo cha Darajani Zanzibar yataanza Oktoba 20, 2025 na udahili wa wanafunzi ukitaraji kuanza wiki ijayo.  “Tumefungua Chuo Cha Ufundi pale Kituo Cha Darajani ghorofa ya pili na kozi zitazofundishwa kwa wanafunzi wa dini zote ni Makeup, Information Communication and Technology (ICT), English Language, French, Secretarial, Tourism, Event Planning Management, Food and Baverage Services zitafundishwa bure kwa vijana wote waliomaliza kidato cha nne na darasa la saba na kushin...

WAHANDISI WASIOFANYA KAZI KWA WELEDI WAFUTIWE LESENI NA WASIPEWE TENA MIRADI;ULEGA

Image
  Waziri wa ujenzi Abdallah Ulega amesema wahandisi wasiofanyakazi kwa weledi na uadilifu na nidhamu wanapaswa kufutiwa leseni zao na kutopewa miradi yeyote ya kijamii. Hayo ameyasema leo Septemba 26,2025 jijini Dar es Salaam wakati akifunga Maazimisho ya 22 ya siku ya wahandisi yaliyokuwa na kauli mbiu isemayo 'wajibu wa wahandisi kuelekea dira ya maendeleo 2050'. Amesema miradi isipotekelezwa vyema inaharibu taaluma na kupelekea kupoteza imani kwa wananchi hali inayopelekea taswira mbaya kwa Taifa. "Naagiza kwa msisitizo mkubwa wahandisi wasiofanya kazi kwa uadilifu na nidhamu bila kufuata viapo vyao wasipewe kazi tena na wachukuliwe hatua kali",Amesema Ulega. Aidha imeipongeza ERB kwa kuandaa kongamano hili muhimu kwa mustakabali wa taifa huku akihisii bodi hiyo kuyapeleka mapendekezo yote waliyoyajadili ili serikali iweze kuyashughulikia kwa haraka. "Nina uhakika kwa makini sana mada zote saba ambazo mlikuwa nazo hivyo hakikisheni mapendokezo yote yalitotokan...

TAALUMA YA UHANDISI NI INJINI YA MAENDELEO-DK.BITEKO

Image
  Na.Sophia Kingimali. NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko, amesema taaluma ya uhandisi moyo wa taifa kwani Taifa haliwezi kupiga hatua za haraka za maendeleo bila kuwekeza kwa dhati katika taaluma ya uhandisi huku akisisitiza kuwa sekta hiyo ni injini ya ukuaji wa viwanda na maendeleo ya teknolojia. Akizungumza leo Septemba 25,2025 jijini Dar es Salaam wakati wa akifungua wa Maadhimisho ya 22 ya Siku ya Wahandisi, ambapo alimwakilisha Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Dkt. Biteko alibainisha kuwa tafiti zinaonesha kila dola moja inayowekezwa katika uhandisi huzalisha kati ya dola saba hadi kumi. “Kama taifa linataka kupiga hatua za haraka, haliwezi kuacha kuwekeza katika taaluma ya wahandisi kwani Dunia nzima inatambua kuwa taaluma hii ndiyo moyo wa maendeleo ya nchi,” amesema Dkt. Biteko. Amesema  kuwa zaidi ya asilimia 70 ya wabunifu wapya katika teknolojia duniani wanatokana na taaluma ya uhandisi, huku akiitaja sekta ya nishati na akili bandia kama mifano y...

MASANJA ATANGAZWA RASMI KUWA BALOZI WA MWANGAZA,AIOMBA SERIKALI KUSAPOTI WAWEKEZAJI WA NDANI.

Image
Mtumishi wa Mungu, mtangazaji na msanii maarufu nchini, Emmanuel Mgaya(Masanja Mkandamizaji) ametangazwa rasmi kuwa balozi wa kampuni ya Kitanzania ya Mwangaza Stationery & Supply kwa lengo la kuwaelimisha Watanzania kuhusu matumizi ya vifaa bora na vya kisasa vya maofisini. Pia,ametoa rai kwa serikali na taasisi zake zote nchini pamoja taasisi binafsi kuhakikisha wanaagiza vitendea kazi vya ofisini kwao kutoka kwa Mwangaza kwani hufanya hivyo ni kuendelea kutoa fursa za ajira kwa vijana lakini kusapoti uwekezaji wa ndani Akizungumza baada ya kusaini makubaliano hayo Septemba 24,2025 jijijini Dar es salaam Masanja amesema ameamua kushirikiana na Mwangaza kutokana na ubora wa bidhaa zao na huduma makini wanazotoa kupitia vijana wenye weledi. "Kiukweli, kupitia Mwangaza, kile kilio cha watu wanaohitaji vifaa vya ofisini vyenye ubora wa hali ya juu kitapatiwa suluhisho. Vifaa vyao vina viwango vya kimataifa na vinapatikana kwa bei nafuu," alisema Masanja. Aidha, aliwahimiza ...

SERIKALI YAONDOA VAT KWA VITUO VYA GESI ASILIA ILIYOSHINDILIWA (CNG)

Image
  📌 *Lengo ni kuongeza uwanda wa  matumizi ya CNG katika vyombo vya moto nchini* 📌 *Mhandisi Mramba azindua kituo cha Gesi Asilia iliyoshindiliwa ( CNG) cha PUMA Energy* 📌 *Asema vifaa vya kuwekea mifumo  ya gesi  kwenye vyombo vya moto pia imeondolewa* 📌 *Apongeza PUMA Energy kwa kuiunga mkono Serikali katika ujenzi wa vituo vya CNG* Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba amesema  Serikali imeondoa kodi ya ongezeko la thamani  (VAT) kwa vituo vyote vya Gesi iliyoshindiliwa (CNG) nchini  ili kuhamasisha matumizi ya gesi asilia  kwenye vyombo vya moto kupitia uwepo wa vituo vingi vya kutoa huduma hiyo kwa wananchi.  Amesema kuwa Serikali pia imeondoa kodi kwenye vifaa vya kuwekea mifumo hiyo ya gesi  kwenye vyombo vya moto kama vile magari na bajaji ikiwa ni hatua pia ya kuhamasisha matumizi ya gesi asilia katika vyombo vya moto. Mhandisi Mramba ameeleza hayo leo Septemba 24, 2025 jijini Dar es Salaam wakati  aki...

WAHANDISI VIJANA WAASWA KUWA CHACHU YA AJIRA KWA VIJANA WENZAO.

Image
Na Sophia Kingimali. Naibu katibu Mkuu wizara ya ujenzi Dk Charles Msonde ametoa rai kwa wahandisi vijana nchini kutumia taaluma yao kujiajili na kuajili wenginie lakini kuhakikisha pia wanaweza kutumia taaluma hiyo kutatua changamoto mbalimbambali zinazolikabili Taifa. Wito huo ameutoa leo Septemba 24,2025 Jijini Dar es salaam wakati akifunga kongamano la siku mbili la wahandisi vijana(YEF )liliangaliwa na bodi ya wakandarasi(ERB) Amesema jukwaa hilo ni la kipekee kwani limekuwa na faida kwa mtu mmoja mmoja lakini pia kwa jamii na Taifa kwa ujumla hivyo vijana wanapaswa kuzingatia ambayo wamefundishwa kwa muda huo wa siku mbili. "Tunapohitimisha jukwaa hili tunapaswa tukumbuke mbegu mpaka iote ni lazima ioze hivyo niwasihi kutokata tamaa ukifanya kwa mara ya kwanza usipofanikiwa usikate tamaa jaribu tena mpka upate suluhisho ya unachokifanya",Amesema Dk.Msonde. Akizungumzia kuhusu ukuaji wa teknolojia amesema kufuatia na ukuaji wa teknolojia ni vyema kuwepo na majukwaa hayo ...

MAANDALIZI YA UCHAGUZI MKUU 2025 IRINGA YAPAMBA MOTO, VIFAA VYAENDELEA KUPOKELEWA

Image
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele leo Septemba 22, 2025 ametembelea  Halmashauri ya Manispaa ya Iringa katika Jimbo la Iringa Mjini na Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo  jimbo la Kilolo Mkoani Iringa ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kukagua maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 ambapo pamoja na mambo mengine alipokea taarifa ya majimbo hayo kutoka kwa wasimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri kuhusu maandalizi ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa Mwaka 2025 na kisha kukagua vifaa ambavyo tayari vimepokelewa katika Halmashauri hiyo.   Jaji Mwambegele pia alipata fursa ya kushuhudia Kampeni za Mgombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha Makini (MAKINI), Mhe. Coster Jimmy Kibonde na Mgombea Mwenza, Mhe.  Aziza Haji Suleiman waliokuwa katika Mkutano wa Kampeni Stendi ya Zamani ya Mkoa wa Iringa majira ya Saa 10 jioni.  Kwa mujibu wa ratiba il...