Posts

Showing posts from November, 2025

MNDEJEMBI AWAHAKIKISHIA WAKAZI WA KIGAMBONI UMEME WA UHAKIKA*

Image
  📌Afanya Ziara katika Kituo cha Dege  📌Aelekeza hatua za haraka kuchukuliwa kunusuru hali ya umeme Kigamboni 📌Umeme wa Megawati 22 kupatikana kwa hatua za haraka  📌Upanuzi wa Kituo cha Dege wafikia asilimia 60  Waziri wa Nishati Mhe. Deogratius Ndejembi amefanya ziara ya kikazi ndani ya Mkoa wa kitanesco wa Kigamboni na kuagiza kuchukuliwa hatua za haraka za kuhakikisha hali ya umeme katika Mkoa wa Kigamboni inaboreshwa na kuwapa wakazi wa eneo hilo huduma ya uhakika alipotembelea Kituo cha Kupokea, Kupoza na Kusambaza umeme cha Dege tarehe 29 Novemba, 2025. “Leo tumekuja kuona ni namna gani Shirika letu la TANESCO linaweza kutatua changamoto hii kwa haraka zaidi na wameweka mipango mizuri ya muda mrefu katika kuhakikisha wanawezesha kupatikana kwa umeme wa uhakika kwa kujenga na kukiongezea nguvu Kituo cha Dege kwa kuweka transfoma ya MVA 120”, ameeleza Mhe. Ndejembi.  Ili kukabiliana na changamoto ya huduma ya umeme iliyopo kwa haraka, Shirika limekuja na...

MRADI WA UMEME KISHAPU KIELELEZO CHA ONGEZEKO LA UZALISHAJI UMEME NCHINI – DC KISHAPU

Image
  📌Mradi wa umeme wa jua wafikia asilimia 84 ya utekelezaji 📌MD Twange aagiza ukamilishwe ifikapo Januari 15, 2026 Mkuu wa Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Peter Masindi, amesema mradi wa umeme unaozalishwa kwa nguvu ya jua ni kielelezo cha ongezeko la uzalishaji wa umeme nchini  ikiwa ni dhamira ya Serikali ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ya kutaka kuongeza uzalishaji umeme hadi kufikia jumla ya megawati 8000 ifikapo mwaka 2030. Masindi aliyasema hayo Novemba 28, 2025, alipoambatana na Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, kukagua maendeleo ya Mradi wa kuzalisha umeme wa jua unaotekelezwa wilayani humo. Amesema mradi huo sio tu utakuwa na faida kwa wananchi wa Mkoa wa Sinyanga pekee bali hadi katika mikoa ya Jirani ambapo pia amesema zaidi ya wananchi 1,200 waliokuwa wakiendesha shughuli zao katika eneo la Mradi tayari  wamelipwa fidia na kwamba jamii imeupokea mradi kwa mtazamo chanya na imekuwa mstari wa mbele kulinda miundombinu. “Mradi huu ni tegeme...

WAZIRI AIPONGEZA BRELA KWA KUBORESHA MIFUMO NA KUONGEZA UFANISI.

Image
  Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Salvio Kapinga, ameipongeza Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) kwa hatua kubwa za kuboresha mifumo ya utoaji huduma ili kuendana na dira ya Serikali katika masuala ya Biashara na Uwekezaji. Akizungumza katika ziara yake aliyoifanya kwenye ofisi za BRELA, leo tarehe 27 Novemba 2025 Mhe. Kapinga alisema Serikali inaendelea kushuhudia mapinduzi makubwa ya kiteknolojia kwenye sekta ya viwanda, hivyo ni muhimu taasisi zinazohusiana moja kwa moja na biashara kuendelea kuboresha huduma zake. "Tuko kwenye mapinduzi makubwa ya kiteknolojia, katika kipindi kama hiki huwezi kuacha kuzungumzia teknolojia inayorahisisha mazingira ya kufanya biashara. Nawapongeza kwa maboresho makubwa ya mifumo ambayo imeleta tija kwa kiasi kikubwa," alisema Waziri Mhe. Kapinga Aidha, alieleza kuwa mpango wa maendeleo wa nchi unakusudia kuifikisha Tanzania kwenye uchumi wa trilioni dola na kwamba hilo linawezekana kwa kuweka mazingira rafiki ya kufa...

WANANCHI TOENI TAARIFA SAHIHI MNAPOKWENDA KUJISAJILI NIDA:KAJI.

Image
  Na.Sophia Kingimali.Dar es salaam. Wananchi wametakiwa kutoa taarifa sahihi wanapokwenda kujisajili katika Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), ili kuepusha usumbufu na changamoto zinazoweza kujitokeza baadaye, wakati wa kufanya marekebisho ya taarifa zao. Wito huo umetolewa leo Novemba 27,2025  jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mkuu wa NIDA James Kaji wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kibali maalum kilichotolewa na Serikali kwa ajili ya kushughulikia maombi ya mabadiliko ya taarifa. Amesema huduma ya mabadiliko ya taarifa imekuwa ikitolewa kwa watu waliojiandikisha katika mfumo wa NIDA kwa kufuata sheria, kanuni na miongozo iliyopo. Amefafanua kuwa kwa kipindi kirefu, NIDA ilipokea maombi mengi ya mabadiliko ya taarifa ambayo hayakuweza kushughulikiwa kutokana na kutokidhi matakwa ya kisheria na taratibu zilizokuwapo ambapo baadhi ya maombi hayo yalitoka kwa watu waliotumia nyaraka za kughushi au kutoa taarifa za udanganyifu walipojisajili, jambo lililo...

NDEJEMBI: TANZANIA SASA INA UMEME WA KUTOSHA.

Image
  *📌 Akagua mradi wa JNHPP: Asema ujenzi wa njia ya umeme Chalinze – Dodoma unaendelea* *📌 Atoa rai kwa watanzania kulinda vyanzo vya maji ili mradi wa JNHPP uendelee kupata mtiririko wa maji ya kutosha* *📌 MD TANESCO asema Serikali inatekeleza miradi ya umeme yenye thamani ya sh. trilioni 13.5* 📍 JNHPP Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema Tanzania kwa sasa ina umeme wa kutosha na hivyo ukamilifu wa Mradi wa kufua umeme wa Julius Nyerere umeondoa kabisa mgao wa umeme nchini. Mhe. Ndejembi ameyasema hayo leo Novemba 26, 2025 wakati wa ziara yake katika Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) iliyoleng kujionea namna mradi huo unavyozalisha umeme na kujihakikishia kuwa uzalishaji unaendelea kwa ufanisi kama ilivyopangwa.  Waziri Ndejembi amesema kuwa tayari mradi wa Julius Nyerere umekamilika na una uwezo wa kuzalisha Megawati 2,115, kiwango ambacho kimeleta uthabiti wa upatikanaji wa nishati na kupunguza changamoto za upatikanaji umeme zilizokuwa zi...

WAZIRI WA KAZI NA UWEKEZAJI ZANZIBAR ASIFU TUZO ZA WATENDAJI AZITAJA KUWA KIVUTIO CHA UWEKEZAJI.

Image
  Na Mwandishi Wetu. Waziri wa Kazi na Uwekezaji Zanzibar, Shariff Ali Shariff Asema tuzo za Wakuu na Watendaji wa Makampuni 100 Bora Kuvutia Uwekezaji na kukuza uchumi wa Tanzannia. Waziri Shariff aliyasema hayo wakati akishiriki hafla ya utoaji tuzo hizo zilizofanyika 21 Novemba 2025 katika ukumbi wa The Super Dome Masaki Dar es salaam na kuhudhuliwa na watendaji mbalimbali "Tuzo hizi zimekuwa kivutio kikubwa cha uwekezaji nchini hali inayopelekea uchumi wetu kama nchi kukua lakini na utendaji kazi wa makampuni mbalimbali kuimalika",Amesema Shariff.

TANESCO MMEFANYA MAGEUZI MAKUBWA KATIKA HUDUMA YA UMEME KWA WANANCHI – NDEJEMBI

Image
  📌 Aelekeza kuongeza kasi na ubunifu katika kuunganishia wananchi umeme 📌 Asisitiza hatua kali za kisheria kwa wakandarasi wazembe 📍 Dodoma Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeendelea kufanya mageuzi makubwa katika kuboresha upatikanaji wa  huduma ya umeme nchini hatua ambayo imeongeza imani na fursa mbalimbali za kiuchumi kwa wananchi. Ndejembi ameyasema hayo Novemba 22, 2025, mkoani Dodoma katika kikao chake na viongozi wa TANESCO chenye lengo la kufanya tathmini na kukumbushana majukumu muhimu ya kuwahudumia wananchi. Ameutumia mkutano huo kuwataka watendaji wa TANESCO kuongeza kasi na ubunifu katika kuwaunganishia wananchi umeme kama sehemu ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Misheni 300. Amesema kuwa ili mpango huo utekelezeke ipasavyo, ni lazima kuwachukulia  hatuaza kisheria  wakandarasi wote watakaobainika kuwa wazembe au kushindwa kuendana na kasi ya serikali ya kuhakikisha kila Mtanzania ananufaik...

MKUU WA WILAYA MISENYI AWABORESHEA MAZINGIRA YA BIASHARA VIJANA NA WANAWAKE MPAKA WA MUTUKULA.

Image
  Na Mwandishi wetu. Mkuu wa Wilaya ya Misenyi Hamisi Mayamba Maiga, amezindua rasmi mahema maalumu ya kuboresha mazingira ya biashara kwa vijana na wanawake katika mpaka wa Mutukula, mkoani Kagera. Mradi huo unatekelezwa na TCCIA kwa ushirikiano na AGRA, ukiwa na lengo la kukuza biashara za mpakani na kuongeza usalama wa shughuli za kiuchumi. ‎Uzinduzi huo ni mwendelezo wa utekelezaji wa mradi unaoendelea katika mikoa mbalimbali nchini, ambapo tayari umefanyika Kigoma na sasa umefika Kagera. ‎Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mhe. Maiga aliipongeza TCCIA na AGRA kwa juhudi za kuwawezesha wafanyabiashara wadogo, hususan vijana wanaojishughulisha na biashara za mazao, mboga mboga na matunda katika maeneo ya mipakani. ‎“Kwanza nitoe pongezi sana kwa TCCIA na AGRA kwa kuandaa mradi huu na kuutekeleza kwa viwango. Hii ni fursa kubwa kwa vijana wetu, hasa hawa wa mpakani,” alisema. ‎“Serikali inaunga mkono jitihada hizi; endeleeni kuzifikisha katika mipaka yote nchini.” ‎Aidha, aliwatak...

Viongozi wa Serikali katika mitaa na kata ni chachu ya maendeleo:DC Mpogolo.

Image
 Na Sophia Kingimali Mkuu wa wilaya wa Ilala Edward Mpogolo amesema serikali inatambua na kuthamini Ushirikiano unaoendelea kati ya viongozi wa serikali za mitaa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), katika kuhakikisha huduma za umeme zinawafikia wananchi kwa wakati na kwa ufanisi.  Hayo ameyasema leo Novemba 20,2025 wakati akifungua  mafunzo maalumu kwa viongozi wa kata na mitaa,  Amesema viongozi wa serikali za mitaa wana nafasi ya kipekee katika kusimamia masuala ya umeme kwa kuwa wao ndio wapo karibu na wananchi hivyo viongozi wanapaswa kuwasaidia wananchi kufahamu hatua sahihi za kutoa taarifa za hitilafu za umeme kupitia mfumo mpya wa Nihudumie, ambao unatoa huduma kwa haraka na bila gharama. "Viongozi ni watu muhimu katika kusimamia ulinzi wa miundombinu ya umeme, ikiwemo nguzo na nyaya, hasa katika maeneo ya mijini ambayo yanakabiliwa na uharibifu kutokana na shughuli za ujenzi ambapo baadhi ya uharibifu huo husababishwa na watu wanaounganisha umeme kiholel...

NECTA:MAANDALIZI MTIHANI KIDATO CHA NNE YAKAMILIKA,MTIHANI KUANZA KUFANYIKA OCTOBA 17.

Image
  Na Sophia Kingimali,Dar es salaam. Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limethibitisha kukamilika kwa maandalizi yote ya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) unaotarajiwa kuanza Novemba 17 hadi Desemba 5, 2025, katika vituo 5,868 vya shule na 813 vya watahiniwa wa kujitegemea.  Akizungumza na waandishi wa habari leo Nov 16,2025 jijini Dar es salaam Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Prof. Said Mohamed, amesema maandalizi yamefanyika kwa umakini ili kuhakikisha mtihani unafanyika kwa amani na uadilifu. "Kwa mwaka 2025, jumla ya watahiniwa 595,816 wamesajiliwa kufanya mtihani huo, wakiwemo 569,914 wa shule na 25,902 wa kujitegemea. Kati ya watahiniwa wa shule, wasichana ni 303,886 sawa na asilimia 53.32, huku wavulana wakiwa 266,028 sawa na asilimia 46.68. Aidha, watahiniwa 1,128 wa shule na 56 wa kujitegemea ni wenye mahitaji maalum, hatua ambayo imeifanya NECTA kuweka miundombinu maalum ya kuwawezesha kufanya mtihani bila vikwazo",Amesema  Prof.Mohamed Akifafanua umuhimu wa ...

SERIKALI YAJIDHATITI KUENDELEA KUIBORESHA SEKTA YA HORTICULTURE

Image
  Na.Sophia Kingimali. Serikali  imesema itaendelea na jitihada zake za kukuza sekta ya horticulture kama injini muhimu ya mageuzi ya kiuchumi, ajira, kipato na mauzo ya nje.  Kauli hiyo imetolewa leo Novemba 12,2025 Jijini Dar es salaam na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Dk. Jim Yonazi, kwa niaba ya Katibu Mkuu Kiongozi, wakati akifungua  Mkutano wa Biashara na Uwekezaji wa Horticulture (HoBIS2025). Dk. Yonazi amesema katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, Serikali imefanya mageuzi makubwa ya kimuundo na kisera yaliyolenga kuboresha mazingira ya uwekezaji na kuongeza ushindani wa kimataifa wa mazao ya horticulture. Alibainisha kuwa kuanzishwa kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) ni miongoni mwa hatua zilizosaidia kurahisisha usimamizi na maendeleo ya sekta hiyo. Aidha, amesema Serikali imeboresha sera za kodi na biashara, kuimarisha Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), na kujenga miundombinu muhimu kama umwagiliaji, maghala ya barid...

VETA Furahika Yazindua Kozi Mpya kwa Ajili ya Vijana Nchini.

Image
  Na Sophia Kingimali. Mkuu wa Chuo cha VETA Furahika, Aliko Mmongele, amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kuchaguliwa tena kuongoza taifa, sambamba na Makamu wa Rais Dk. Nchimbi, huku akieleza kuwa serikali imeendelea kuonyesha dhamira ya dhati ya kuwawezesha vijana kupitia elimu ya ufundi. Akizungumza chuoni hapo leo Novemba 6,2025 Jijini Dar es salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari Mmongele amesema pongezi hizo zinaenda sambamba na jitihada za serikali kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) katika kuimarisha elimu ya ufundi stadi nchini, jambo linalosaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana. “Kwa niaba ya uongozi wa VETA Furahika, napenda kumpongeza Mheshimiwa Rais na Makamu wake pamoja na Rais wa Zanzibar kwa uongozi bora na sisi Tumejipanga kuunga mkono juhudi zao kwa kuhakikisha vijana wanapata mafunzo yatakayowasaidia kujiajiri,” amesema Mmongele. Amefafanua kuwa chuo hicho kimeanzisha ...

TUME YATANGAZA WABUNGE 115 WA VITI MAALUM

Image
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani, Jacobs Mwambegele (katikati) akiongoza kikao cha Tume kilichokutana Jijini Dodoma leo Novemba 7, 2025 na kupitisha majina ya wabunge wa viti maalum. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Tume , Mhe. Jaji wa Rufaa (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk na kushoto ni Katibu wa Tume ambae pia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Ramadhani Kailima.  Tume ikiwa katika kikao chake hii leo.  ************** Kwa kuzingatia masharti ya Ibara ya 66(1)(b) na 78(1) za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 zikisomwe pamoja na kifungu cha 112 cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya Mwaka 2024, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi katika kikao chake kilichofanyika leo tarehe 07 Novemba, 2025 imefanya uteuzi wa Wabunge Wanawake wa Viti Maalumu 115 kati ya idadi ya Wabunge 116 wanaopaswa kuteuliwa.  Aidha, nafasi ya Mbunge mmoja uteuzi wake utafanyika baada ya kukamilisha uchaguzi wa Ubunge katika Jimbo l...