Posts

Showing posts from January, 2026

Wanafunzi wanaokwenda kusoma nje ya nchi wafundwa.

Image
 Na. Sophia Kingimali Wito umetolewa kwa wanafunzi wanaokwenda kusoma nje ya nchi kutumia fursa wanazopewa kwa nidhamu, bidii na kuzingatia maadili, ili wakirejee walete mchango chanya kwa maendeleo ya Taifa. Wito huo umetolewa leo Januari 30,2026 katika hafla ya kuwaaga wanafunzi 16 kati ya 50 wa programu ya Samia Scholarship Extended DS/AI, iliyoandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, amewasisitiza wanafunzi hao kuwa mabalozi wa nchi na kuhakikisha wanajifunza kwa bidii, wanaheshimu sheria za nchi wanazoenda "Mkatumie maarifa mtakayopata kuleta suluhisho la changamoto za maendeleo hapa nchini ili kupata mabadiliko chanya kulingana na dira ya maendeleo ya 2050",Amesema Prof. Mkenda. Profesa Mkenda amesema programu ya Samia Scholarship ni matokeo ya dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuwekeza kwenye sayansi, teknolojia na rasilimali watu, hususan kwa vijan...

BoT yaimarisha usimamizi wa akiba ya taifa, yauza ziada ya dhahabu kupunguza vihatarishi

Image
  Na.Mwandishi Wetu. BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imeeleza kuwa hatua ya kuuza sehemu ya dhahabu iliyopo kwenye hifadhi yake inalenga kuimarisha usimamizi wa akiba ya taifa na kupunguza vihatarishi vya kifedha, badala ya kufadhili miradi ya maendeleo ya serikali kama ilivyodhaniwa na baadhi ya wadau. Akizungumza na waandishi wa habari leo January 30,2026  jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Idara ya Masoko ya Fedha wa BoT, Emmanuel Akaro, amesema Bodi ya Benki hiyo imeweka kiwango cha juu cha hifadhi ya dhahabu kisichozidi thamani ya Dola za Marekani bilioni mbili, huku kiwango cha sasa kikiwa kimefikia takribani dola bilioni 3.2. Akaro amesema ziada hiyo ndiyo inayopangwa kuuzwa ili kurejesha uwiano sahihi wa muundo wa hifadhi ya fedha za kigeni, hatua inayolenga kuhakikisha akiba ya taifa inabaki salama na inayoweza kutoa faida kupitia uwekezaji wa kimataifa. Amefafanua kuwa fedha zitakazopatikana zitawekezwa kwenye masoko ya fedha ya kimataifa ili kuongeza mapato ya uwekezaj...

NECTA YAIPONGEZA SERIKALI KWA KULETA MAGEUZI SEKTA YA ELIMU

Image
  Na. Sophia Kingimali. Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA)Profesa Said Mohammed,amesema kuwa juhudi za Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan zimeleta mageuzi makubwa katika sekta ya elimu, hususan katika kuimarisha stadi za msingi za KKK (Kusoma, Kuandika na Kuhesabu) kwa wanafunzi wa elimu ya awali na msingi.  Akizungumza leo Januari 29,2026 Jijini Dar es salaam wakati wa hafla ya uzinduzi wa mpango Mkakati wa kisayansi wa kujenga umahiri wa kusoma,kuandika na kuhesabu KKK, kwa wanafunzi wa awali,darasa la kwanza na la pili amesema tukio hilo ni la kihistoria na linaonesha dhamira ya dhati ya Rais katika kuboresha elimu nchini. Ameeleza kuwa mpango wa KKK unalenga watoto wa miaka mitano hadi saba, ambao ni umri wa msingi katika kujenga uwezo wa kujifunza.  "Endapo mtoto hatapata stadi hizo mapema, huathirika katika nyanja zote za ukuaji ikiwemo kiakili, kijamii na kihisia. Kwani hali hiyo ni sawa na mtoto mchanga anayekosa mazi...

RAIS DKT. SAMIA AZINDUA MPANGO MKAKATI WA KKK AWATAKA WAANGALIZI WA ELIMU NCHINI KUSIMAMIA UTEKELEZAJI WAKE.

Image
  Na Sophia Kingimali-Dar es salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa wito kwa waangalizi wa elimu nchini kusimamia kwa karibu utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Kisayansi wa Kujenga Umahiri wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK),huku akisisitiza kuwa mpango huo usibaki kwenye makaratasi bali utoe matokeo halisi kwa watoto wa awali pamoja na wanafunzi wa darasa la kwanza na la pili. Wito huo ameutoa leo Januari 29,2026  wakati wa uzinduzi wa mpango huo jijini Dar es Salaam, Rais Samia ame sema lengo kuu la mkakati huo ni kuhakikisha hakuna mtoto anayefika darasa la tatu bila kuwa na uwezo wa msingi wa kusoma, kuandika na kuhesabu, kwani stadi hizo ndizo msingi wa mafanikio ya masomo katika ngazi zote za elimu. Aidha Rais Samia ameipongeza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI pamoja na wadau wa maendeleo kwa maandalizi ya mpango huo, akisema jitihada hizo zinaonesha dhamira ya dhati ya S...

BRELA YAENDELEZA MKAKATI WA KUSOGEZA HUDUMA ZAKE KWA WANANCHI, NJOMBE..

Image
  Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imeendelea na mkakati wake wa kuwafikia wafanyabiashara kwenye maeneo yao kwa kuwasogezea huduma zote muhimu za urasimishaji biashara, kutoa elimu na kutatua changamoto zinazowakabili wafanyabiashara wa mkoa wa Njombe. Hatua ya kusogeza huduma za papo kwa papo kwa wananchi inalenga kuwaondolea changamoto za kupata huduma za Usajili wa Kampuni, Majina ya Biashara, Utoaji wa Leseni za Biashara Kundi A, Utoaji wa vyeti na Leseni za Viwanda, Usajili wa Alama za biashara na Huduma pamoja na Utoaji wa hataza. Awali akiwakaribisha Maafisa wa BRELA ofisini kwake, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe (RAS), Muhandisi. Joseph Rutashubilwa, aliipongeza  BRELA na kusema kuwa mkakati huo unawaweka wadau wake karibu zaidi na kwamba ni fursa adhimu kwa wananchi wa mkoa wa Njombe. Aidha, Muhandisi. Rutashubilwa alitumia nafasi hiyo kuwahimiza wananchi wa maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Njombe, hususan Njombe Mjini, Makambako, Ludewa na Makete ku...

TANESCO YAFANYA UKAGUZI WA MITA KITAALAMU KUBAINI UKWELI MALALAMIKO YA UMEME KUISHA HARAKA YAGUNDUA MITA ZIPO SAWA*

Image
  📌 Ni kufuatia malalamiko ya baadhi ya wateja kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari 📌 Chanzo cha tatizo kwa mita zilizokaguliwa chatajwa kuwa ni uchakavu wa wiring za ndani ya nyumba na tabia holela za matumizi ya umeme 📌 Shirika kuongeza kasi ya utoaji wa elimu ya matumizi bora ya umeme kwa wananchi. Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limefanya ukaguzi wa kitaalamu wa mita za umeme kwa baadhi ya wateja waliowasilisha malalamiko hayo kwa njia za mitandao katika maeneo ya Tabata Kimanga na Kimara Suka jijini Dar es Salaam. Malalamiko hayo yaliibuliwa na baadhi ya wananchi mitandaoni na kwenye vyombo vya habari kuhusu madai ya umeme kuisha haraka bila sababu ya msingi. Zoezi hilo lilifanyika Januari 27, 2026, likiongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Bi. Irene Gowelle, akiambatana na timu ya wataalamu wa Shirika, kwa lengo la kubaini chanzo halisi cha changamoto hiyo na kujiridhisha kuhusu ufanisi wa utendaji wa mita za wateja. *Ma...

WAZEE DAR WAWATAKA GEN Z KUDUMISHA AMANI, WAMPONGEZA RAIS SAMIA SIKU YA KUMBUKIZI YA KUZALIWA

Image
  Na Mwandishi Wetu. Baadha ya Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam wametoa wito mzito kwa vijana wa kizazi cha Gen Z kudumisha upendo na amani, wakisema kuwa hiyo ndiyo misingi ya maendeleo ya Taifa,  Wito huo wameutoa leo Januari 27,2026 Jijini Dar es salaam wakati wa hafla ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, iliyoandaliwa na taasisi ya Vijana innovation na kuratibiwa na taasisi ya Together for Samia. Wazee hao wamesema kuwa Tanzania imebarikiwa amani kubwa inayotamaniwa na mataifa mengi, hivyo vijana wanapaswa kuwa walinzi wakuu wa tunu hiyo kwa kuishi kwa upendo, mshikamano na kuepuka vitendo vinavyoweza kuvuruga utulivu wa nchi. Akizungumza kwa niaba ya wazee, bi Sophia amesema kuwa wao kama wazee wataendelea kuliombea Taifa, lakini vijana nao wana wajibu wa kuhakikisha amani inatawala kwa vitendo, kwani bila amani hakuna maendeleo wala ustawi wa kweli. “Ni nchi ya amani, tusivuruge amani tuliyopewa na Mwenyezi ...

NAIBU WAZIRI SALOME AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA WIKI YA NISHATI INDIA 2026.

Image
  Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, leo Januari 27, 2026 ameshiriki katika ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Nishati India (India Energy Week – IEW 2026), yanayolenga kujadili na kuweka mikakati ya pamoja ya kukuza sekta ya nishati kwa njia endelevu na shirikishi, sambamba na kubainisha fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo katika nchi washirika pamoja na namna bora ya kuzifikia. Maadhimisho hayo yamefunguliwa rasmi na Waziri Mkuu wa India, Mhe. Narendra Modi, katika Jimbo la Goa nchini India, na yanahudhuriwa na washiriki kutoka zaidi ya nchi 125 duniani, wakiwemo viongozi wa serikali, wataalamu wa nishati, wawekezaji na wadau wa sekta binafsi. Katika maadhimisho hayo, Mhe. Salome ameambatana na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini India, Mhe. Balozi Anisa Mbega, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Dkt. James Andilile, Kamishna Msaidizi wa Maendeleo ya Umeme kutoka Wizara ya Nishati, Mha. Styden Rwebangila, pamoja ...

WATENDAJI WA UCHAGUZI WATAKIWA KUTEKELEZA MAJUKUMU KWA WELEDI

Image
Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk akizungumza leo tarehe 26 Januari, 2026 mkoani Iringa wakati akifunga mafunzo ya siku tatu ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe.(Picha na INEC). Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk akizungumza leo tarehe 26 Januari, 2026 mkoani Iringa wakati akifunga mafunzo ya siku tatu ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe. Meza Kuu ikiongozwa na Mwenyekiti wa Tume, Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele ikiwa katika ufungaji wa mafunzo hayo. Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakifuatilia hotuba ya ufungaji mafunzo yao ya siku tatu. Washiriki wa ma...

𝗞𝗔𝗪𝗔𝗜𝗗𝗔: 𝗡𝗜𝗠𝗣𝗢𝗡𝗚𝗘𝗭𝗘 𝗥𝗔𝗜𝗦 𝗗𝗞𝗧. 𝗦𝗔𝗠𝗜𝗔 𝗞𝗨𝗘𝗡𝗗𝗘𝗟𝗘𝗔 𝗞𝗨𝗟𝗘𝗧𝗔 𝗠𝗔𝗘𝗡𝗗𝗘𝗟𝗘𝗢

Image
  Mwenyekiti wa UVCCM na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Ndugu Mohammed Ali Kawaida amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuendelea kuleta maendeleo hususani ahadi alizotoa katika kampeni za Uchaguzi Mkuu katika siku 100 za kwanza za uongozi wake. Ndugu Kawaida akizungumza na maelfu ya wanafunzi wa Vyuo vya Kati na Vyuo Vikuu mkoani Dodoma leo tarehe 24 Januari 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete. Ametaja baadhi ya yaliyotekelezwa ikiwemo Bima ya Afya kwa wote na ajira kwa vijana zikiwemo za udaktari.

HANANG YAPANDA MICHE 350 YA MITI SHULENI, TFS YAANIKA MPANGO WA MICHE 1,100 KUMUENZI RAIS SAMIA

Image
  Hanang, 23 Januari 2026 Jimbo la Hanang limepiga hatua kubwa katika uhifadhi wa mazingira baada ya Mbunge wa Hanang, Mh. Asia Halamga, kwa kushirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) – Hanang, kupanda miche 350 ya miti ya matunda na kivuli katika Shule ya Sekondari Chief Sarja, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha mazingira ya kijani na kukuza lishe bora kwa jamii. Zoezi hilo limewakutanisha viongozi mbalimbali wa serikali, wanafunzi wa shule hiyo pamoja na wananchi, na kuonyesha mshikamano wa dhati kati ya uongozi wa umma na wananchi katika kulinda mazingira na kuboresha ustawi wa jamii kupitia upandaji miti unaozingatia faida za lishe na kivuli. Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Mh. Halamga alisisitiza umuhimu wa ushiriki wa jamii katika mapambano dhidi ya uharibifu wa mazingira, akieleza kuwa upandaji wa miti ya matunda ni mkakati unaochangia moja kwa moja afya na kipato cha wananchi sambamba na uhifadhi wa mazingira. Kwa upande wake, Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Mlima H...