Posts

Showing posts from March, 2026

MHANDISI MATIVILA AKAGUA MIRADI YA DMDP II, ATOA WITO UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU

Image
  πŸ“ŒTARURA kujenga takribani Km. 250 za barabara Manispaa zote za Dar es Salaam ‎ ‎Dar es Salaam ‎ ‎Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila, amesema Serikali kupitia TARURA inaendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa mradi wa Uboreshaji wa Miundombinu mkoa wa Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP II) huku akiwataka wananchi kushiriki kikamilifu katika utunzaji wake ili idumu kwa muda mrefu. ‎Ameyasema hayo ‎wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa mradi wa DMDP II katika Manispaa za Ubungo na Kinondoni, akisisitiza umuhimu wa kukamilika kwa miradi hiyo kwa wakati ili kuboresha miundombinu na maisha ya wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam. ‎Mhandisi Mativila alikagua miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa barabara ya Msumi Km 9.9 na daraja la Msumi na ujenzi wa barabara ya Goba Wakorea km 7.76 zilizopo Ubungo pamoja na ujenzi wa barabara ya Mivumoni Km 4.79 iliyopo Kinondoni ambapo uteke...

KAMATI YA BUNGE YAPITISHA RANDAMA YA MADINI MWAKA 2026/27.

Image
  ✅️ Madini Yachangia Asilimia 57 ya Mauzo Yote ya Bidhaa Zisizo za Asili Nje ya Nchi ✅️ Makusanyo mpaka Februari 2026 Yafikia Shilingi Bilioni 880 ✅️ GST Yakidhi Vigezo Kuendelea Kuwa na Ithibati Mpaka 2029 ✅️ Waziri Mavunde Asisitiza Ununuzi wa Helikopta ya Utafiti, Mipango Iko Pale Pale πŸ“ Dodoma Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini leo Machi 26, 2026 imepitisha Randama ya Wizara ya Madini kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya kawaida na maendeleo kwa mwaka wa fedha 2026/27 katika kikao kilichofanyika jijini Dodoma, ambacho pia kimepokea taarifa ya utekelezaji wa Wizara kwa kipindi cha Julai 2025 hadi Februari 2026 kwa mwaka 2025/26. Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Subira Mgalu, ameipongeza Wizara kwa namna inavyosimamia utekelezaji wa majukumu yake yaliyopelekea kuongeza mchango wa sekta ya madini kwenye Pato la Taifa kufikia asilimia 12.7 katika robo ya tatu ya Julai hadi Septemba 2025, ikiwemo kuibua miradi mipya na shughuli za ut...

PBPA YAAGIZWA KUHARAKISHA UPOKEAJI NA USAZAMBAZAJI WA MAFUTA NCHINI.

Image
  Dar es Salaam Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius John Ndejembi ameutaka Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) kuhakikisha kuwa maghala yote makubwa ya usambazaji wa mafuta yanapata bidhaa hiyo kwa wakati, ili kuimarisha upatikanaji wake nchini. Hayo yamesemwa  leo Machi 26, 2026 jijini Dar es Salaam wakati wa kikao chake na viongozi wa PBPA, Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) na kampuni ya TIPER kwa lengo la kujadili hali ya upokeaji wa mafuta yanayoingia nchini. Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Ndejembi ameielekeza PBPA kuweka mfumo madhubuti wa upangaji wa ratiba ya ushushaji wa mafuta (sequencing) ili kuhakikisha maghala yote makubwa yanayohusika na usambazaji yanapata mafuta kwa usawa na kwa wakati.  Amesema hatua hiyo itasaidia kupunguza changamoto za upatikanaji wa mafuta katika maeneo mbalimbali ya nchi. Aidha, ameeleza kuwa Serikali imekubaliana kuharakisha ushushaji wa meli za mafuta zinazoingia nchini, hususan kwa ajili ya matum...

NDEJEMBI ATAKA EWURA KUKAGUA MAGHALA YA MAFUTA KUHAKIKISHA HAKUNA MAFUTA YANAYOFICHWA.

Image
  πŸ“Œ*Asema nchi ina usalama mkubwa wa mafuta hivyo wananchi waendelee kupata huduma muda wote* πŸ“Œ*Timu maalum kuundwa kufuatilia uingizaji wa mafuta nchini* Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi ameitaka Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kuhakikisha kuwa, hakuna mfanyabiashara anayeficha mafuta kwa kisingizio cha kusubiri bei za mafuta zipande kutokana na mgogoro unaoendelea katika eneo la Mashariki ya Kati ambao umepelekea baadhi ya nchi kukumbana na changamoto za upatikanaji wa mafuta. Akizungumza jijini Dodoma katika kikao na Taasisi za Wizara zinazosimamia Sekta ya Mafuta, Mhe. Ndejembi ameeleza kuwa nchi ina usalama mkubwa wa mafuta na kwamba Serikali imejipanga vizuri kuhakikisha  wananchi katika maeneo yote wanapata huduma bila vikwazo hivyo EWURA anapaswa kuhakikisha hakuna mafuta yanayofichwa katika maghala ya kuhifadhi Mafuta. Aidha, ili kuhakikisha mafuta yote yaliyoagizwa nje ya nchi yanafika nchini kwa mujibu wa mkataba, Mhe. Ndejembi ...

TANESCO YAGUSA MIOYO YA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

Image
  πŸ“ŒNi sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii  πŸ“ŒYatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar es Salaam. Katika kuendeleza dhamira ya uwajibikaji kwa jamii, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), tarehe 19 Machi 2026, lilifanya ziara ya kutembelea vituo vitatu vya watoto wenye mahitaji maalum jijini Dar es Salaam, na kutoa misaada mbalimbali kwa lengo la kuleta faraja na matumaini. Akizungumza wakati wa ziara hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji ,Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Bi. Irene Gowelle, alisema kuwa lengo la ziara hiyo ni kushirikiana na jamii kwa vitendo kwa kutoa misaada hususan kwa makundi ya watoto yenye uhitaji . Alieleza kuwa msaada huo haujalenga tu kukidhi mahitaji ya msingi, bali pia kuwajengea watoto hao imani, matumaini na ujasiri wa kuendelea kuamini katika ndoto zao licha ya changamoto wanazokabiliana nazo. “Leo TANESCO tumeshiriki na watoto hawa wenye mahitaji maalum kwa kutoa misaada mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya kurejes...

MAKAMU WA RAIS AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA MISITU DUNIANIA NA KAMPENI YA UPANDAJI MITI KITAIFA.

Image
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ameelekeza uongozi wa Mikoa yote nchini kuhakikisha jitihada za upandaji miti zinaendelezwa kwa kuwekewa mkakati mahsusi unaojumuisha makundi yote katika jamii na kuzingatia ikolojia ya maeneo husika, ikiwa ni pamoja na kuzuia uvamizi na uharibifu wa maeneo yote ya hifadhi ya misitu.   Makamu wa Rais, ametoa maelekezo hayo, wakati akifungua Maadhimisho ya Siku ya Misitu Duniani na Siku ya Upandaji Miti Kitaifa, iliyofanyika katika Uwanja wa Ilulu mkoani Lindi, leo tarehe 19 Machi 2026. Amesema ni muhimu kuhakikisha wananchi wanaoishi jirani na misitu ya asili na mashamba ya miti wanapatiwa elimu endelevu kuhusu matumizi bora ya ardhi, udhibiti wa uchomaji moto holela, na usimamizi shirikishi wa misitu ya vijiji.   Aidha, Makamu wa Rais amehimiza umuhimu wa Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI) kufanya tafiti zitakazojibu changamoto mbalimbali...

Utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24 zijazo.

Image
 

JOWUTA yapitishwa rasmi kuwa mwanachama wa CoRI.

Image
  Na Mwandishi Wetu CHAMA cha Wafanyakazi katika Vyombo vya Habari Tanzania (JOWUTA), kimepitishwa  rasmi kuwa mwanachama wa Taasisi ya Wadau Wanaopigania Haki za kupata Habari (CoRI). JOWUTA wamepitishwa na CoRI katika kikao chake cha tatu kilichofanyika Desemba 5 mwaka jana, baada ya chama hicho kutuma maombi ya kujiunga kutokana na jukumu lake kubwa la kutetea na kulinda maslahi na uhuru wa wafanyakazi katika vyombo vya habari Tanzania. Mwenyekiti wa CoRI, Ernest Sungura amesema wanachama wa taasisi hiyo wametambua mchango mkubwa wa JOWUTA kupigania haki za waandishi wa habari, kuhamasisha usimamizi wa sheria ya habari, kujengea uwezo wa kitaaluma na kupigania uhuru na maadili ya uandishi, jambo ambalo linaendana na dhumuni la CoRI. "Tunawakaribisha CoRI tushirikiane kupigania sekta ya habari ili iweze kusonga mbele zaidi kwa pamoja,"amesema. Mwenyekiti wa JOWUTA, Mussa Juma amesema uamuzi wa CoRI kupokelewa kuwa mwanachama una faida kubwa kwa JOWUTA ambayo ina wanachama z...

TANESCO yazindua Drones kuboresha ukaguzi wa miundombinu ya umeme nchini

Image
  Na.Mwandishi wetu. *Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia za kidigitali *Drones hizo kutumika kukagua njia za usafirishaji na usambazaji umeme nchini Shirika la Umeme Tanzania, TANESCO, limezindua rasmi matumizi ya ndege nyuki (drones) kwa ajili ya kufanya ukaguzi wa njia za kusafirisha na kusambaza umeme ikiwa ni hatua inayolenga kuongeza ufanisi wa utoaji huduma na kupunguza muda wa kutatua changamoto za kukatika kwa umeme. Uzinduzi huo umefanyika Machi 17, 2026 katika Ofisi za TANESCO, Ubungo jijini Dar es Salaam, ukiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo, Lazaro Twange. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Twange amesema TANESCO inasimamia mtandao mkubwa wa miundombinu ya umeme nchini unaohitaji ufuatiliaji wa karibu kwa kutumia teknolojia za kisasa. “Tuna njia za kusafirisha umeme ambazo zimetembea urefu wa takribani kilomita 8,500, na tuna njia za kusambaza umeme ambazo zimetembea karibu kilomita 200,000. Njia hizi zi...

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI YAIPONGEZA TANESCO UTEKELEZAJI WA MRADI WA UMEME JUA KISHAPU

Image
  Na.Mwandishi wetu. πŸ“Œ Watembelea mradi kuona ufanisi wake πŸ“Œ Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi πŸ“Œ Watoa rai awamu ya pili kuanza kwa kasi Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imelipongeza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa usimamizi na utekelezaji mzuri wa Mradi wa Uzalishaji Umeme kwa nguvu ya Jua wa Kishapu wenye uwezo wa Megawati 50 unaotekelezwa katika Mkoa wa Shinyanga. Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Subira Mgallu, mara baada ya Kamati kutembelea mradi huo tarehe 13 Machi, 2026 kwa lengo la kujionea maendeleo ya utekelezaji wake pamoja na ufanisi wa matumizi ya fedha zilizotolewa na Serikali. Akizungumza mara baada ya ziara hiyo, Mhe. Mgallu alisema mradi huo ni hatua muhimu katika mageuzi ya sekta ya nishati nchini kutokana na matumizi ya teknolojia ya nishati jadidifu. “Tumetembelea mradi huu wa uzalishaji wa umeme kwa kutumia teknolojia ya jua na tunaona ni mapinduzi makubwa katika sekta ya nishati nchini. Hii ni hat...

Tanesco kufanya maboresho mfumo wa luku.

Image
 

Wanawake TANESCO waaswa kuwa mabolozi wazuri wa nishati safi ya kupikia.

Image
 Na.Sophia Kingimali. Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima, ametoa wito kwa wanawake watumishi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuwa vinara wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, akisisitiza kuwa wao ndio mabalozi muhimu wa mabadiliko kuanzia ngazi ya familia hadi taifa. Akizungumza leo March 4,2026 jijini Dar es salaam katika kongamano la wanawake wa TANESCO, Waziri Gwajima amesema shirika hilo lina mchango mkubwa katika maendeleo endelevu ya taifa na ustawi wa wanawake, hasa kupitia upatikanaji wa umeme unaorahisisha maisha na kuinua uchumi wa familia.  Ameipongeza kamati ya maandalizi kwa kufanikisha kongamano hilo na kueleza kuwa limekuja wakati muafaka kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake. Waziri gwajima ameitaja ajenda ya nishati safi ya kupikia ni ya kitaifa na haiwezi kufanikiwa bila ushiriki wa sekta zote, akiwemo wanawake wa TANESCO huku  akisisitiza kuwa bila umeme wa uhakika katik...