Posts

Showing posts from December, 2025

WANANCHI FUONI WAJITOKEZA KUPIGA KURA KUCHAGUA MBUNGE WAO

Image
Mkazi wa Shehia ya Migombani katika jimbo la Fuoni akipiga kura leo kumchagua Mbunge wa jimbo hilo.  Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taiofa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele akiwa na mkazi wa Shehia ya Fuoni aliyekua akihakiki jina lake kabla ya kuingia kupiga kura leo.  Mjumbe wa Tume, Mhe. Magdalena Rwebangira akizungumza mmoja wa wasimamizi wa viuo vya kupigia Kura katika jimbo la Fuoni Mjini Zanzibar leo.  Mkazi wa Shehia ya Migombani katika jimbo la Fuoni akipiga kura leo kumchagua Mbunge wa jimbo hilo katika kituop cha Skuli ya Raudha B.  Mwenyekiti wa Tume na Mjumbe wa Tume hiyo wakizungumza na Mawakala katika moja ya vituo vya kupigia Kura.  Wananchi wa Jimbo la Fuoni na Siha pamoja na Kata tano za Tanzania bara wamejitokeza kwawingi kupiga kura leo Desemba 30,2025 katika Uchaguzi mdogo uliofanyika katika majimbo yao. Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele leo Desemba 30,2025 ametembelea na kushuhudi...

VIONGOZI WA DINI WAASWA KUTUMIA STAHA KWENYE KUKEMEA MAOVU.

Image
  Na.Sophia Kingimali. Muumini wa Kanisa Katoliki, Mwalimu Ludovick Joseph, amesema viongozi wa dini wana haki na wajibu wa kiroho kukemea maovu yanapotokea katika jamii ili kujenga dhamiri za waumini na kutoa mwelekeo wa kimaadili kwa Taifa. Akizungumza na waandishi wa habari leo Disemba 30,2025 katika tafakari yake kwa umma, Mwalimu Ludovick amesema kauli za viongozi wa dini kuhusu masuala nyeti ya kijamii na kitaifa ni halali, kwani zina mchango mkubwa katika kuhimiza haki, amani na maadili mema miongoni mwa waumini na jamii kwa ujumla. Hata hivyo, amesema kasoro kubwa inayojitokeza ni matumizi ya lugha, akisisitiza kuwa uongeaji wa viongozi wa dini haupaswi kufanana na lugha ya wanasiasa au wapinzani wa kisiasa, bali uwe wa kidini, kichungaji na wa kimaadili. Amefafanua kuwa viongozi wa dini wanapaswa kutumia lugha ya upendo, maridhiano na hekima, huku wakiepuka kauli zinazoweza kuchochea migawanyiko au kuleta taharuki katika jamii. Pia amekosoa wingi wa matamko kutoka kwa vion...

WANANCHI SIHA ,FUONI KATA TANO KUPIGA KURA KUCHAGUA WABUNGE NA MADIWANI LEO

Image
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele leo Desemba 29,2025 amesoma risala maalum kuhusu uchaguzi wa ubunge katika jimbo la Siha lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Siha, Mkoa wa Kilimanjaro, Tanzania Bara na Jimbo la Fuoni lililopo Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini Magharibi, Tanzania Zanzibar unaotaraji kufanyika Desemba 30,2025.   Jaji Mwambegele amesema, uchaguzi mdogo huo utahusisha pia, kata tano za Tanzania Bara. Kata hizo ni;            Chamwino iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Mkoa wa Morogoro; Mbagala Kuu iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Temeke, Mkoa wa Dar es Salaam; na Nyakasungwa iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa, Mkoa wa Mwanza.   Nyingine ni Kata ya Masoko iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Mkoa wa Mbeya; na kata ya Ndono iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Uyui, Mkoa wa Tabora.   Aidha, amesema jumla ya wago...

Waumini wa Kanisa Katoliki watoa tamko dhidi ya kauli za Askofu Rwaichi.

Image
  Na Mwandishi Wetu. Waumini wa Kanisa Katoliki, McDonald Silinde na Gerald Abel, wametoa tamko kwa vyombo vya habari wakilaani kauli walizodai zilitolewa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddeus Ruwa’ichi, wakati wa mahubiri ya Misa ya Krismasi iliyofanyika Desemba 25, 2025. Akisoma tamko hilo mbele ya  waandishi wa habari leo Disemba 27,2025 Jijini Dar es Salaam, MacDonald Silinde amesema wametoa tamko hilo kwa huzuni na masikitiko makubwa, wakieleza kuwa maneno yaliyotamkwa madhabahuni yamewaumiza waumini wengi kisaikolojia na kiimani, na kuvunja misingi ya mafundisho ya Kikristo. Silinde amesisitiza kuwa madhabahu ya kanisa ni mahali patakatifu pa kuhubiri Neno la Mungu, kuimarisha imani na kuleta faraja, na si jukwaa la matusi, vitisho au lugha ya chuki dhidi ya waumini. Kwa mujibu wao, maneno makali na ya kudhalilisha yaliyodaiwa kutumiwa na Askofu, yakiwataja waumini kwa misemo kama “wapumbavu” na “wasaliti”, hayana nafasi katika mahubiri ya ...

WAJASILIAMALI DSM WALAANI MAANDAMANO NA VURUGU WAAHIDI KUSHIRIKI KWENYE ULINZI WA AMANI.

Image
  Na.Mwandishi wetu Wajasiriamali wa mkoa wa Dar es Salaam wamelaani vikali maandamano na vurugu za Oktoba 29, wakisisitiza kuwa vitendo hivyo vimeathiri kwa kiasi kikubwa biashara zao, ajira na ustawi wa jamii, huku wakitangaza kujipanga kulinda amani na mshikamano wa taifa. Tamko hilo limetolewa leo jijini Dar es Salaam na wawakilishi wa wafanyabiashara kutoka wilaya zote tano za mkoa huo ambazo ni Ilala, Temeke, Ubungo, Kinondoni na Kigamboni, mbele ya waandishi wa habari, wakisema amani ndiyo msingi wa maendeleo na uchumi wa huduma unaotegemewa na wakazi wa jiji hilo. Akizungumza kwa niaba ya wajasiriamali wa Ilala, Selemani, mfanyabiashara wa vifaa vya michezo kutoka Mboto, alisema kuwa bila amani hakuna biashara, hakuna ajira na hakuna maendeleo, hivyo kundi hilo limeazimia kupaza sauti kupinga vurugu na uchochezi wa aina yoyote. Selemani aliongeza kuwa wajasiriamali wanapinga vikali watu wanaohamasisha machafuko wakiwa nje ya nchi au kupitia mitandao ya kijamii, akisema mara...

VIONGOZI WA DINI,WANASIASA NA VIONGOZI WA SERIKALI ACHENI KUTOA MATAMKO SUBIRINI MATOKEO YA TUME;MCHUNGAJI MASHIMO.

Image
  Wito umetolewa kwa viongozi wa dini na serikali kuacha kutoa matamko kufuatia matukio yaliyotokea Oktoba 29, badala yake wasubiri matokeo ya tume iliyoundwa kuchunguza tukio hilo. Wito huo umetolewa leo Disemba 23,2025 Jijini Dar es salaam na Mchungaji Daud Mashimo wakati akizungumza na waandishi wa habari. "Ni muhimu kwa taifa kujipa muda wa kutafakari na kusubiri majibu ya mamlaka husika ili kuepusha kuchochea hisia na migawanyiko miongoni mwa wananchi, akisisitiza kuwa amani na utulivu ndio msingi wa mshikamano wa Taifa",Amesema. Akizungumza kwa hisia, mchungaji huyo amewataka viongozi wa dini za madhehebu yote kusimama pamoja na kuwa sauti ya faraja kwa Watanzania, badala ya kuendelea kufufua maumivu ya matukio ya nyuma ambayo yanaweza kuzaa chuki na mpasuko wa kijamii. Katika hotuba yake, Mashimo amempongeza Katibu wa Baraza la TEC, Padre Kitime, kwa mchango wake mkubwa katika kulijenga taifa kupitia maneno ya busara na faraja, akisema amekuwa sauti muhimu kwa Watanzan...

SERIKALI KUENDELEA KUTOA FURSA KWA MAKUNDI MAALUM:DK GWAJIMA.

Image
 Na Sophia Kingimali. Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima, amesema Serikali inaendelea kutekeleza kwa kasi shughuli za maendeleo na kutoa fursa mbalimbali kwa makundi maalum ikiwemo wanawake, vijana, watoto, wazee na wafanyabiashara ndogondogo katika mwaka wa fedha 2025/26. Akizungumza na waandishi wa habari leo Disemba 22,2025 jijini Dar es salaam, Dkt. Gwajima amesema jitihada hizo zinafanyika chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa lengo la kujenga Taifa jumuishi lenye haki, usawa na ustawi wa wananchi wote. "Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 inalenga kuwekeza zaidi katika sekta zinazotoa ajira kwa wingi zikiwemo kilimo, utalii, viwanda, ujenzi, michezo, sanaa za ubunifu na madini, hatua itakayoongeza fursa za kiuchumi kwa makundi maalum"Amesema Dk Gwajima.  Sambamba na hayo amewahamasisha wananchi kutumia vyuo vya maendeleo ya jamii vilivyopo maeneo mbalimbali nchini pamoja...

WAZIRI KOMBO AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KUSHIRIKI KATIKA MKUTANO WA PILI WA JUKWAA LA MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE WA NCHI ZA AFRIKA NA URUSI ULIOFANYIKA TAREHE 19 NA 20 DISEMBA, 2025, JIJINI CAIRO, MISRI

Image
  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo, ameongoza Ujumbe wa Tanzania kushiriki katika Mkutano wa Pili wa Jukwaa la Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi za Afrika na Urusi uliofanyika tarehe 19 na 20 Disemba, 2025, jijini Cairo, Misri. Mkutano huo ulihudhuriwa na Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Afrika, Jumuiya za Kikanda za Afrika pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi.  Mkutano huo uliofanyika chini ya Wenyeviti Wawili, Mheshimiwa Dkt. Badr Abdelatty, Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri na Mhe. Sergey Lavrov, Waziri wa Mambo ya Nje wa Shirikisho la Urusi, umetoa nafasi ya nchi za Afrika na Urusi kujadiliana na kukubaliana masuala muhimu yanayogusa maslahi ya pamoja katika nchi zao na katika Umoja wa Mataifa, na Mashirika yake. Mawaziri wa Afrika na Urusi wamesisitiza umuhimu wa Umoja wa Mataifa na Mashirika yaliyo chini yake, ikiwemo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kufanyiwa marekebisho ili kuongeza uwakilishi wa Afrika...

KATAMBI AITAKA BRELA KUWEKA MKAZO WA ELIMU KWA VIJANA

Image
  Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara,  Patrobas Katambi, ameitaka Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) kuimarisha utoaji wa elimu kwa umma ili kufikisha taarifa kwa Watanzania, hususan vijana, kuhusu namna ya kurasimisha biashara zao na kupata leseni za biashara. Katambi ametoa maelekezo hayo leo, tarehe 18 Desemba, wakati wa ziara yake katika ofisi za BRELA alipokutana na Menejimenti ya Wakala, ambapo alieleza kuwa kwa sasa Serikali imeelekeza nguvu kubwa katika kuwawezesha vijana. “Katika usajili wa kampuni na maeneo ya biashara, suala la elimu ni muhimu zaidi na linapaswa kupewa kipaumbele. Ni muhimu kuhakikisha taarifa zinawafikia Watanzania kuhusu mabadiliko yanayotokea, huduma mpya zinazoanzishwa pamoja na maeneo yanayowakwaza zaidi wafanyabiashara katika usajili, ili yapatiwe ufumbuzi na elimu itolewe ipasavyo,” amesema Mhe. Katambi. Aidha, ameongeza kuwa Serikali imetenga asilimia 30 ya tenda zote zinazotolewa kwa ajili ya kampuni zinazomilikiwa na vijana, ...

Mhe Kapinga azihimiza kampuni kuhuisha taarifa kwa Msajili wa Kampuni.

Image
  Judith Kapinga, Waziri wa Viwanda na Biashara amezihimiza  kampuni zinazofanya biashara nchini kuendelea kuhuisha taarifa zao kwa Msajili wa Kampuni ili zisaidie kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara nchini, mifumo ya usajili na utoaji wa leseni, sheria zinazosimamiwa na  Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) na kuweza kushirikiana na Taasisi nyingine hususan Mamlaka za serikali za mitaa na mamlaka za udhibiti kwa kuunganisha mifumo ya utoaji huduma ili kuondoa urasimu wa utoaji huduma kwa wateja.    Wito huo umetolewa leo tarehe 18 Desemba, 2025 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya utekelezaji wa majukumu ya wizara ya viwanda na biashara katika ofisi za idara ya habari-MAELEZO jijini Dar es Salaam.  Mhe Kapinga ameeleza kuwa taasisi ya BRELA iliyochini ya Wizara yake imefanikiwa na inaendelea kuunganisha mifumo yake na mifumo ya Taasisi nyingine ambapo Mfumo wa Usajili kwa njia ya Mtandao (ORS) umeunganishwa na jumla ya Taasis...

MABORESHO YA SERA NA SHERIA SEKTA YA VIWANDA YAZAA MATUNDA.

Image
  Na.Sophia Kingimali,Dar es salaam SERIKALI imeeleza kuwa maboresho ya sera na sheria katika sekta ya viwanda na biashara yameanza kuzaa matunda, yakiongeza uzalishaji, ajira na ushindani wa bidhaa za Tanzania katika masoko ya ndani na nje ya nchi. Akizungumza na waandishi wa habari Leo Disemba 18,2025 jijini Dar es salaam Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga, amesema mwelekeo wa sasa unaonesha sekta hiyo ikibadilika kutoka utegemezi wa bidhaa za nje kwenda uzalishaji wenye tija na thamani iliyoongezwa. Kapinga amesema mchango wa sekta ya viwanda katika Pato la Taifa umefikia zaidi ya asilimia 7.3 huku biashara ikichangia asilimia 8.6 mwaka 2024, hali aliyoitaja kuwa ishara ya kuimarika kwa mazingira ya biashara na upanuzi wa masoko. Aidha amebainisha kuwa mauzo ya nje ya bidhaa na huduma yameongezeka hadi kufikia zaidi ya dola za Marekani bilioni 16.8, yakichangiwa na bidhaa za viwandani na kilimo zilizoongezewa thamani. Aidha Waziri huyo ameongeza kuwa uzalishaji mkubwa...

MECIRA YATAKA USHIRIKIANO WA KIDIPLOMASIA KUDHIBITI UHAMASISHAJI WA VURUGU

Image
  Na.Sophia Kingimali. KITUO cha Wanahabari Watetezi wa Rasilimali na Taarifa (MECIRA) kimehimiza jumuiya ya kimataifa kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia na kisheria katika kudhibiti uhamasishaji wa vurugu unaofanyika kupitia mipaka ya nchi, kikisisitiza kuwa hatua hizo ni muhimu kulinda amani na mshikamano wa Tanzania. Akizungumza leo Disemba 17,2025 jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa MECIRA, Habibu Mchange, amesema kituo hicho tayari kimeziarifu Serikali za Marekani na Kenya kuhusu uwepo wa watu wanaotumia nchi hizo kama majukwaa ya kusambaza taarifa potofu na kuchochea machafuko dhidi ya Tanzania. Mchange amesema kuwa ingawa Tanzania inatambua na kuheshimu misingi ya demokrasia, haki za binadamu na uhuru wa kujieleza, misingi hiyo haiwezi kutumika kama kisingizio cha kuhalalisha vitendo vinavyohatarisha maisha ya watu au kuvuruga amani ya taifa jingine. Amesisitiza kuwa uhuru wa kujieleza una mipaka ya kisheria na lazima uendane na uwajibikaji, hasa pale unapovuka mipaka ya...

MWENYEKITI WA BODI YA WAKURUGENZI TANESCO AKABIDHIWA RASMI OFISI.

Image
  📌Asema TANESCO imepiga hatua kubwa katika utekelezaji wa miradi ya umeme 📌Apongeza jitihada zinazoendelea za  kuimarisha eneo la huduma kwa wateja  📌Aahidi kutoa ushirikiano na kuendeleza alipoishia mtangulizi wake Mwenyekiti  wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Bw. Plasduce Mbossa, leo Desemba 16, 2025 amekabidhiwa rasmi ofisi na aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi hiyo,  Mhe. Dkt. Rhimo Nyansaho, ambaye kwa sasa ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Hafla hiyo ya makabidhiano imefanyika jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi pamoja na Menejimenti ya TANESCO. Akizungumza katika hafla hiyo, Bw. Mbossa amesema Mheshimiwa Nyansaho ameondoka akiiacha  TANESCO katika mwelekeo mzuri  na usimamizi mzuri baada ya miradi mingi mikubwa ya umeme kukamilika ikiwemo miradi ya kimkakati kama Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere ambalo limechangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha uzalishaji na upatik...