Posts

Showing posts from April, 2026

FURAHA KWA WATEJA CRDB: WASHINDA SAFARI YA KOMBE LA DUNIA 2026, WENGINE WATINGA NA TV ZA KISASA INCHI 85.

Image
  Na Mwandishi Wetu Furaha na shangwe vimetawala kwa baadhi ya Watanzania baada ya kujikuta wakishinda zawadi nono kupitia kampeni ya “Tembo Card Visa” ya Benki ya CRDB, huku wanne wakipata nafasi ya kipekee ya kusafiri kwenda Marekani kushuhudia fainali za Kombe la Dunia 2026. Washindi hao, waliopatikana kupitia droo ya kwanza iliyochezeshwa jijini Dar es Salaam, wameeleza hisia zao za mshangao na furaha, wakisema hawakutarajia kupata nafasi hiyo adhimu katika maisha yao. Miongoni mwa washindi wa safari hiyo ni Kenneth Masana Bina kutoka Kagera, Gasper Melkiory Kavishe wa Morogoro, pamoja na wakazi wa Dar es Salaam Arnold John Samugabo na Erick Harison Mlinga. Mbali na safari hiyo ya kihistoria, washindi wengine watatu walijishindia runinga janja (Smart TV) za inchi 85 pamoja na dishi na kifushi, wakisema zawadi hizo zitabadilisha namna wanavyofurahia burudani majumbani mwao. Akizungumza mara baada ya droo hiyo, Meneja Mwandamizi wa Kitengo cha Kadi wa CRDB, Karington Chahe, amese...

Njia Mpya za Usafirishaji Mirungi Zafichuliwa, Serikali Yaonya Kuongezeka kwa Mtandao wa Baharini.

Image
  Na Mwandishi wetu, Pwani MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imebaini kuibuka kwa njia mpya za usafirishaji wa dawa za kulevya kwa kutumia bahari, kufuatia kukamatwa kwa boti ya mwendokasi iliyokuwa ikisafirisha mirungi kutoka Mombasa, Kenya hadi Bagamoyo mkoani Pwani. Operesheni hiyo iliyofanyika usiku wa kuamkia Aprili 14, 2026 katika ufukwe wa Magambani, eneo la Kaole Ufundi, ilipelekea kukamatwa kwa viroba 18 vyenye paketi 1,062 za mirungi pamoja na watuhumiwa wanne wanaodaiwa kuhusika na mtandao huo. Akizungumza leo Aprili14,2026 Bagamoyo Pwani, Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo, amesema tukio hilo linaonesha mabadiliko ya mbinu zinazotumiwa na wasafirishaji wa dawa za kulevya, ambapo sasa wanatumia njia za baharini kukwepa ulinzi uliopo nchi kavu. Alisema boti hiyo imekuwa ikifuatiliwa kwa muda mrefu, ikihusishwa na usafirishaji wa mirungi kutoka Mombasa kuja Dar es Salaam, hali inayothibitisha kuwepo kwa mtandao mpana unaoratibiwa kuvusha dawa...

MJUMBE WA JUMUIA YA MADOLA RAIS MSTAAFU CHAKWERA AKUTANA NA INEC

Image
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) ikiongozwa na Mwenyekiti wa Tume, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele leo Aprili 14, 2026 amekutana na kuzungumza na mjumbe maalum Jumuiya ya Madola (Commonwealth) Rais wa zamani wa Malawi Mhe.Lazarus McCarthy Chakwera ambaye alitembelea ofisi za Tume Njedengwa jijini Dodoma. Ziara hiyo maalum ya mjumbe huyo wa Jumuia ya Madola ililenga kuangalia namna Uchaguzi Mkuu wa 2025 ulivyofanyika. (Picha na INEC).

Mitandao mipya ya dawa za kulevya yaibuliwa; DCEA yaonya matumizi ya mbinu za kisasa usafirishaji

Image
  Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imebaini kuibuka kwa mitandao mipya ya usafirishaji wa dawa za kulevya inayotumia mbinu za kisasa kuficha bidhaa hizo haramu, hali inayozua tahadhari mpya kwa vyombo vya usalama na wananchi. Akizungumza jijini Dar es Salaam, Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo, amesema wahalifu wameanza kutumia njia zisizo za kawaida kusafirisha dawa hizo, ikiwemo kuzificha kwenye mizigo ya nguo za mitumba, matunda kama maembe, pamoja na ndani ya mifumo ya hewa (AC) ya mabasi. Amesema mabadiliko hayo ya mbinu yanakuja kufuatia kuimarishwa kwa udhibiti katika bandari na mipaka, jambo lililowalazimu wahusika wa biashara hiyo kubuni njia mbadala za kusafirisha dawa hizo ndani ya nchi. “Tunashuhudia wahalifu wakibadilika na kuja na mbinu mpya kila wakati, lakini sisi pia tunaendelea kuimarisha mikakati ya kukabiliana nao,” amesema Lyimo. Katika operesheni zilizofanyika mwezi Machi 2026, mamlaka hiyo ilifa...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO APRIL 13/2026

Image
 

Tanzania yang’ara Tuzo za Utalii Duniani, yaingiza vipengele 41.

Image
  Na.Mwandishi wetu.Dar es salaam TANZANIA imeendelea kung’ara katika anga la kimataifa baada ya kuingiza vipengele 41 katika Tuzo za Utalii na Usafirishaji Duniani (World Travel Awards), hatua inayoimarisha nafasi yake kama moja ya vinara wa utalii barani Afrika. Akizungumza, Aprili 11,2026 jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Paulina Mkama, amesema tuzo hizo zinahusisha jumla ya washindani 85 kutoka sekta za umma na binafsi, zikilenga kutambua na kusherehekea ubora wa huduma, kuhamasisha ushindani na kutoa fursa kwa wadau na watalii kupigia kura vivutio bora duniani. Paulina  ameeleza kuwa ushiriki wa Tanzania katika tuzo hizo ni fursa adhimu ya kuitangaza nchi kimataifa na kuiweka katika ramani ya dunia kama kitovu cha utalii.  Ameongeza kuwa taasisi za serikali, ikiwemo TFS na TAWA, zimefanikiwa kuwasilisha vivutio vyake katika kinyang’anyiro hicho. Kwenye kinyang’anyiro hicho , Tanzania imewania nafasi katika vipenge...

Watumishi Tume ya Uchaguzi watakiwa kuepuka uchochezi, wajipanga uchaguzi Isimani.

Image
  Na Mwandishi Wetu, Morogoro Watumishi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia katiba, sheria, kanuni  na taratibu na kuepuka lugha zozote za uchochezi zinazoweza kuleta uvunjifu wa amani na kuhatarisha maisha ya Watanzania. Hayo yamesemwa leo Aprili 11, 2026 na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu), Dkt. James Henry Kilabuko kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt Jimmy Yonaz wakati akifungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, katika kikao kilichoketi Mkoani Morogoro.  “Napenda kuwaasa, kuzingatia katiba, sheria, kanuni  na taratibu mnapotekeleza majukumu ya Tume na kuepuka lugha zozote za uchochezi zinazoweza kuleta uvunjifu wa amani na kuhatarisha maisha ya Watanzania,”alisema Dkt Kilabuko.   Dkt. Kilabuko amesema, taasisi ina malengo yake, upo uwezakano wa kuepusha migogoro ya ndani na nje ya taasisi inayoweza kuathiri utekelezaji wa ma...

VIONGOZI WA SERIKALI NA KIROHO WANG’ARA MAADHIMISHO YA MIAKA 19 YA WRM JIJINI DAR ES SALAAM

Image
  Na.Mwandishi wetu. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Deus Sangu ameongoza viongozi mbalimbali wa serikali na kisiasa kushiriki maadhimisho ya miaka 19 ya Kanisa la WRC yanayoendelea katika kanisa hilo kivule Jijini Dar es salaam. Katika tukio hilo, Sangu aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, Mbunge wa Kivule, Ojambi Massaburi pamoja na Mbunge wa Bunda, Ester Bulaya, ambapo walipokelewa na waumini na viongozi wa kanisa hilo. Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mpogolo alisema kutimiza miaka 19 kwa Kanisa la WRC ni historia kubwa inayostahili pongezi, akiwashukuru pia viongozi wa kanisa hilo  kwa mchango wao mkubwa katika kuimarisha huduma za kiroho na maendeleo ya kijamii katika mkoa huo. Ameongeza kuwa uwepo wa viongozi hao umekuwa chachu ya amani na maendeleo nchini, huku akibainisha kuwa serikali itaendelea kushirikiana na taasisi za kidini katika kujenga jamii yenye mshikamano.  Aidha, amegusia chang...

Watanzania waaswa kudumisha amani ili kumtukuza Mungu.

Image
  Na. Mwandishi wetu. Watanzania wameaswa kudumisha amani na mshikamano kuelekea sikukuu ya pasaka ili kuupokea ufufuko wa yesu kristu kwa roho na kweli Wakati akitoa salamu za pasaka Askofu wa kanisa la WRC ( The word ofvReconciliation church) Askofu Nicklous Siguye Amesema kuwa watanzania ni watu wenye utamaduni wa upole na kupenda amani Aidha ameongeza kwa kusema kuwa kama nchi tunapashwa kuwa wamoja bila kujali itikadi za kidini, kisiasa na kikabila ili kuijenga nchi iliyo na umoja Lakini pia amewataka waamini kujiungamanisha na yesu kristu kwa siku zilizo baki kuanzia leo ijumaa kuu mpaka kufikia pasaka ufufuko wa yesu kristu Jumatatu ya pasaka itakuwa ni siku ya maadhimisho ya miaka 19 ya kanisa la WRC ( The word of Reconciliation Church) na kuwakaribisha Watanzania wote kushiriki kwa pamoja kumtukuza Mungu 

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI APEWA MAAGIZO NA BUNGE,SERIKALI

Image
  Na.Mwandishi wetu. SPIKA wa Bunge Mussa Zungu amemtaka  Mwanasheria Mkuu wa Serikali,Hamza Johari kuchukua   hatua kali dhidi ya Taasisi na Mashirika ambayo yalikaidi ushauri wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika Utekelezaji wa Mikataba ya miradi mbalimbali kama ilivyoripotiwa na mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG  Ameyasema hayo jana Aprili 1,2026 Bungeni Dodoma wakati wa hotuba ya Makadirio ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu katika mwaka wa fedha 2026/27 Wakati huo huo Nae Waziri Mkuu Dkt.Mwigulu Nchemba amemuelekeza Mwanasheria huyo Mkuu kukaa pamoja na Wizara ya  Ardhi na TAMISEMI ili waandae mpango mkakati madhubuti katika kuhakikisha kwamba wanapata ufumbuzi wa kudumu juu ya migogoro ya ardhi inayoongezeka kila siku na kuwa kero  kwa Wananchi.

Huu hapo utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24 zijazo Aprili 2,2026.

Image
 

KAMATI YA MAANDALIZI YA MAONESHO SABASABA 2026 YAKUTANA

Image
  Na.Mwandishi Wetu. Kamati ya Maandalizi ya Maonesho ya Sabasaba 2026 imekutana katika makao makuu ya TanTrade kujadili mikakati ya kuboresha mchakato wa maandalizi ya maadhimisho ya miaka 50 ya SABASABA 2026. Katika kikao hicho, Mkurugenzi wa TanTrade, Dkt. Latifa Khamis, aliwasilisha mkakati wa awali wa maandalizi, ukilenga kuhakikisha maonesho ya mwaka 2026 yanatekelezwa kwa viwango vya juu vya ubora na kuvutia washiriki wengi zaidi kutoka ndani na nje ya nchi. Baada ya mawasilisho hayo, Mwenyekiti wa kikao, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Aristides  Mbwasi, aliridhishwa na hatua zilizofikiwa katika maandalizi ya maonesho. Aidha, alisisitiza umuhimu wa kuongeza kasi ya utekelezaji kwa kuwa maonesho haya ni ya kihistoria na yana nafasi kubwa katika kuchochea maendeleo ya biashara na uchumi wa taifa.

BoT Yabaki na Riba ya Asilimia 5.75 Kukabili Changamoto za Uchumi wa Dunia.

Image
  Na Sophia Kingimali. Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania(BoT) imeendelea kuonesha msimamo wa tahadhari katika usimamizi wa uchumi baada ya kuamua kubakiza kiwango cha Riba ya Benki Kuu (CBR) katika asilimia 5.75 kwa robo ya pili ya mwaka 2026. Uamuzi huo unaakisi jitihada za mamlaka ya fedha kulinda uthabiti wa uchumi huku kukiwa na changamoto zinazoendelea katika mazingira ya uchumi wa dunia, hususan migogoro ya kisiasa inayoathiri biashara na uwekezaji. Kamati ya Sera ya Fedha ya Benki Kuu ilifikia uamuzi huo baada ya kufanya tathmini ya kina ya mwenendo wa uchumi wa ndani na nje, ikibaini kuwa kiwango hicho bado kinafaa katika kipindi cha sasa. Akizungumza leo Aprili 2, 2026, Naibu Gavana wa Benki Kuu anayesimamia Sera za Fedha na Uchumi, Dkt. Yamungu Kayandabila, amesema lengo kuu ni kuhakikisha mfumuko wa bei unaendelea kubaki ndani ya wigo wa asilimia 3 hadi 5. Ameeleza kuwa uthabiti wa riba hiyo pia utasaidia kupunguza madhara yanayotokana na misukosuko ya kiuchumi duni...