PBPA YAHAMASISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA
Na.Mwandishi wetu. Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) umechukua hatua madhubuti ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi kwa kuwagawia watumishi wake majiko ya umeme, ikiwa ni sehemu ya juhudi za makusudi za kuhamasisha mabadiliko ya matumizi ya nishati nchini. Akizungumza katika tukio hilo, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa PBPA, Mhandisi Bruno Tarimo, amesema hatua hiyo inalenga kuimarisha juhudi za taasisi katika kuelimisha jamii kuhusu matumizi ya nishati safi na salama kwa matumizi ya kila siku. Ameeleza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia sera mbalimbali za kitaifa na kimataifa, imeendelea kutambua umuhimu wa nishati safi ya kupikia kama nyenzo muhimu ya kukabiliana na changamoto za kimazingira, kiafya, kijamii na kiuchumi. “PBPA inatekeleza jukumu muhimu katika kusaidia juhudi za Serikali za kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034. Ugawaji wa majiko janja aina ya pressure cooker kwa watumishi ni sehemu ya ...