FURAHA KWA WATEJA CRDB: WASHINDA SAFARI YA KOMBE LA DUNIA 2026, WENGINE WATINGA NA TV ZA KISASA INCHI 85.
Na Mwandishi Wetu Furaha na shangwe vimetawala kwa baadhi ya Watanzania baada ya kujikuta wakishinda zawadi nono kupitia kampeni ya “Tembo Card Visa” ya Benki ya CRDB, huku wanne wakipata nafasi ya kipekee ya kusafiri kwenda Marekani kushuhudia fainali za Kombe la Dunia 2026. Washindi hao, waliopatikana kupitia droo ya kwanza iliyochezeshwa jijini Dar es Salaam, wameeleza hisia zao za mshangao na furaha, wakisema hawakutarajia kupata nafasi hiyo adhimu katika maisha yao. Miongoni mwa washindi wa safari hiyo ni Kenneth Masana Bina kutoka Kagera, Gasper Melkiory Kavishe wa Morogoro, pamoja na wakazi wa Dar es Salaam Arnold John Samugabo na Erick Harison Mlinga. Mbali na safari hiyo ya kihistoria, washindi wengine watatu walijishindia runinga janja (Smart TV) za inchi 85 pamoja na dishi na kifushi, wakisema zawadi hizo zitabadilisha namna wanavyofurahia burudani majumbani mwao. Akizungumza mara baada ya droo hiyo, Meneja Mwandamizi wa Kitengo cha Kadi wa CRDB, Karington Chahe, amese...