CCM KUHUISHA MCHAKATO WA KATIBA MPYA
Mgombea mwenza wa nafasi ya Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt Emmanuel John Nchimbi amesema katika kipindi cha Miaka mitano ijayo, chama hicho kitahuisha Mchakato wa Katiba mpya.
Dkt Nchimbi ametoa kauli hiyo leo Septemba Mosi 2025 wakati akiwa kata ya Dutwa mkoani Simiyu, ikiwa Muendelezo wa Kampeni Kuelekea Uchaguzi mkuu wa Oktoba 29.
Sambamba na mpango huo, pia CCM imedhamiria ndani ya miaka mitano ijayo itaendelea kusimamia na kudumisha Suala la Amani kwa Watanzania.

Comments
Post a Comment