Watanzania waaswa kudumisha amani ili kumtukuza Mungu.
Na. Mwandishi wetu.
Watanzania wameaswa kudumisha amani na mshikamano kuelekea sikukuu ya pasaka ili kuupokea ufufuko wa yesu kristu kwa roho na kweli
Wakati akitoa salamu za pasaka Askofu wa kanisa la WRC ( The word ofvReconciliation church) Askofu Nicklous Siguye Amesema kuwa watanzania ni watu wenye utamaduni wa upole na kupenda amani
Aidha ameongeza kwa kusema kuwa kama nchi tunapashwa kuwa wamoja bila kujali itikadi za kidini, kisiasa na kikabila ili kuijenga nchi iliyo na umoja
Lakini pia amewataka waamini kujiungamanisha na yesu kristu kwa siku zilizo baki kuanzia leo ijumaa kuu mpaka kufikia pasaka ufufuko wa yesu kristu
Jumatatu ya pasaka itakuwa ni siku ya maadhimisho ya miaka 19 ya kanisa la WRC ( The word of Reconciliation Church) na kuwakaribisha Watanzania wote kushiriki kwa pamoja kumtukuza Mungu

Comments
Post a Comment